Thursday, August 31, 2017

EDK:MTAZAMO WA UISLAM JUU YA ELIMU




1.      MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU.
1.1.   Dhana ya Elimu katika Uislamu.
§  Katika Uislamu Elimu maana yake ni:
-          Ujuzi unaoambatana na utendaji au
-          Mabadiliko ya tabia yanayoambatana (yanayotokana) na ujuzi au
-          Ujuzi unaomuwezesha mtu kufanya (kutenda) jambo kwa ufanisi au inavyotakikana.

§ Nani aliyeelimika? (Sifa za mtu aliyeelimika).
-          Aliyeelimika ni yule mwenye ujuzi unaomuwezesha kutenda (kufanya) jambo kwa ufanisi na inavyotakikana.          

-          Mjuzi wa Qur’an na Sunnah ni yule anayeendesha kila kipengele cha maisha yake ya binafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.

-          Watakapo fanana kimwenendo na kitabia wale wenye elimu na wasiokuwa na elimu, basi wenye elimu watakuwa hawajaelimika ila wamesoma tu.

“……………Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua? Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu………”(39:9).

§  Nafasi ya Elimu katika Uislamu.
-          Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika Uislamu inaonekana katika maeneo yafuatayo;
                                            i.            Elimu ndio takrima ya kwanza aliyopewa mwanaadamu na Mola wake kama nyenzo pekee itakayomuwezesha kumjua Mola wake na kumuabudu vilivyo.
“Na (Mwenyezi Mungu) akamfundisha Adam majina ya (fani za) vitu vyote” (2:31) na pia rejea (2:38).

                                          ii.            Elimu ni amri ya kwanza kwa mwanaadamu kuitafuta kama alivyoamrishwa kusoma Mtume (s.a.w).
“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba……..” (96:1-5).

§  Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
1.      Ndio nyenzo pekee inayomuwezesha mwanaadamu kumtambua Mola wake na kuweza kumuabudu ipasavyo.

“Kwa hakika wanaomuogopa (wanaomuabudu) Mwenyezi Mungu ipasavyo miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu” (35:28).

2.      Elimu iliyosomwa kwa murengo wa Qur’an na Sunnah ndio inayomuwezesha muumini kuwa Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni.

“Na kumbukeni aliposema Allah kuwaambia Malaika kwamba ataweka ardhini khalifa (kiongozi)” (2:30) pia rejea (2:38).

3.      Kutafuta elimu ni ibada maalum yenye hadhi kubwa kuliko ibada zote mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) inayopelekea mja kufanya ibada vilivyo.

“……Na (waumini) waliopewa elimu watapata daraja (kubwa) zaidi…” (58:11).

4.      Mwenye elimu ndio ana nafasi bora ya kumtambua na kumuabudu Mola wake ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yake.
Rejea Qur’an (35:28), (39:9) na (58:11).

§  Nini Chanzo cha Elimu?
-          Chanzo cha Elimu na fani zote ni ALLAH (S.W) ambaye humuelimisha mwanaadamu kupitia njia mbali mbali.

o   Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu ni:
1.      Il-hamu.
-     Ni mtiririko wa habari (ujumbe) unaomjia mwanaadamu bila kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yeyote.

2.      Kuongea na Mwenyezi Mungu (s.w) nyuma ya pazia.
-     Ni njia mwanaadamu huongeleshwa na Mwenyezi Mungu (s.w) moja kwa moja kwa sauti ya kawaida bila kumuona.

-     Nabii Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w) nyuma ya pazia.
      Rejea Qur’an (28:30), (7:143) na (19:23-26).

3.      Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa.
-     Ni njia anayoitumia Allah (s.w) kumuelimisha mwanaadamu kwa kupeleka ujumbe kupitia mitume na watu wengine wema.
            Rejea Qur’an (53:1-12), (15:51-66), (19:16-19), (2:102) na (3:41).

4.      Ndoto za kweli (ndoto za mitume).
-     Ni kupata ujumbe kupitia ndoto za kweli hasa kwa mitume ambayo huwa ni maagizo ya Allah (s.w) kwa Mitume.

-   Mfano ndoto ya Nabii Ibrahim (a.s) juu ya kumchinja mwanae Nabii Ismail (a.s).
      Rejea Qur’an (37:102), (12:4-5), (12:100) na (48:27).

5.      Njia ya Maandishi (mbao zilizoandikwa).
-     Ni njia ya mawasiliano ya Allah (s.w) na waja wake kupitia maandishi yaliyoandikwa tayari.

-     Nabii Musa aliletewa ujumbe kwa maandishi kutoka kwa Allah (s.w).
      Rejea Qur’an (7:145) na (7:154).

§  Lengo kuu la elimu katika Uislamu ni;
-          Ni kumuwezesha mwanaadamu kumtambua Mola wake vilivyo na kuweza kumuabudu kwa usahihi na kikamilifu kwa kila kipengele cha maisha yake ya kila siku kibinafsi, kifamilia na kijamii.

-          Ni kuweza kuyajua na kuyafuata maamrisho yote ya Allah (s.w) na kuepukana na makatazo yake pia.


1.2.   Mgawanyo Sahihi wa Elimu kwa Mtazamo wa Uislamu.
 -   Kwa mtazamo wa Uislamu elimu imegawanyika katika nyanja kuu mbili;
a)      Elimu ya Mwongozo (Faradh ‘Ain).
-   Ni elimu ya lazima ambayo kila muislamu (mtu) anapaswa kuisoma, haina uwakilishi. Mfano ibada za swala, funga, hijja, zakat, n.k.

b)     Elimu ya Mazingira (Faradh Kifaya).
-   Ni elimu ya uwakilishi ambapo wakisoma wachache katika jamii inatosheleza    lakini wasipopatikana wa kuwakilisha, jamii yote itawajibika.
Mfano fani ya Udaktari, Uinjinia, Ualimu, Urubani, n.k.


1.3.   Mgawanyo wa Elimu usiokubalika katika Uislamu (usio sahihi).
 -    Katika Uislamu, HAKUNA mgawanyo wa ‘Elimu Dunia’ na ‘Elimu Akhera’.
 -  Mgawanyo huu ni potofu wenye dhana ya kikafiri kuwa kuna maisha ya Dini yanayoongozwa na Mwenyezi Mungu na maisha ya Dunia yanayoongozwa na binaadamu.

·         Mgawanyo huu sio sahihi kwa sababu zifuatazo:
                                      i.      Nabii Adam (a.s) aliandaliwa yeye na kizazi chake kuwa Makhalifa (viongozi) na alifundishwa majina (fani zote) ya vitu vyote.
Rejea Qur’an (2:31) na (2:38-39).

                                    ii.      Amri ya kusoma aliyopewa Mtume (s.a.w) na umma wake haibagui elimu ya dini na dunia.

                                  iii.      Muasisi wa (chanzo cha) elimu na fani zote ni Mwenyezi Mungu (s.w). Hakuna mwanaadamu aliyeasisi elimu au fani yeyote ila ni mwendelezaji tu.
Rejea Qur’an (96:3-5).

                                  iv.      Pia Qur’an inatufahamisha kuwa wanaomcha Allah (s.w) ipasavyo ni waumini wataalamu waliozama katika fani mbali mbali za kumjua Allah (s.w), sio tu fani za kidini za Fiqh, Tawhiid, n.k.
Rejea Qur’an (35:27-28).

                                    v.      Katika Qur’an Allah (s.w) anatufahamisha kuwa waumini wenye elimu ya fani mbali mbali ndio wenye daraja kubwa zaidi mbele yake.
Rejea Qur’an (58:11), (49:13).

                                  vi.      Hakuna mgawanyo wa elimu unaooneshwa katika Hadith za Mtume (s.a.w) zinazoelezea fani za elimu.

  • Elimu yenye Manufaa.
-  Elimu yenye manufaa ni ile yenye sifa zifuatazo:
    1. Ni ile inayomuwezesha mwanaadamu kumtambua na kumuabudu Mola wake vilivyo na ajili ya kufikia lengo la kuumbwa kwake.

    1. Ni ile inayomuwezesha mja (muumini) kuwa Khalifa (kiongozi) wa Allah (s.w) hapa Ulimwenguni.

    1. Ni ile inayoiwezesha jamii kuishi kwa furaha na amani ya kweli.
    2. Ni ile inayotafutwa na kufundishwa kwa ajili ya kupata radhi za Allah (s.w).

  • Mahusiano kati ya elimu ya mwongozo na elimu ya mazingira katika Uislamu.
-   Kusimama na kuendelea kwa Uislamu katika jamii, kunategemea sana uwepo wa elimu zote mbili katika utekelezaji wake.

-  Elimu ya mazingira pekee inapelekea kutofanyika haki na uadilifu katika jamii na kukosekana mwongozo sahihi wa maisha ya jamii.

-     Elimu ya mwongozo pekee pia hupelekea udhaifu katika kuyamudu mazingira kutokana na kukosekana fani mbali mbali za kimaendeleo.









Zoezi la 1.
1.      (a)  Elimu ni nini?
(b)  Mtu aliyeelimika ni mtu wa aina gani?
(c)  Unatoa maoni gani iwapo wanaojua watakuwa sawa na wasiojua kiutendaji?

2.      (a)  “….Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.....(39:9).   Kwa nini wanaojua hawawi sawa na wasiojua?
(b) Kwa kutumia ushahidi wa aya, onesha kuwa elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

3.      Kwa ushahidi wa aya za Qur’an, eleza kwa nini Uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza kabla ya jambo lolote?

4.      (a)  Nini chanzo cha elimu na fani zote?
(b)  “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba…….” (96:1).
      (i)  Kutokana na aya hii, fafanua nini maana ya kusoma ‘kwa jina la Allah’
      (ii) Orodhesha njia tano anazotumia Allah (s.w) katika kuwaelimisha wanaadamu.

5.      (a)  Bainisha ni upi mgawanyo sahihi na usio sahihi juu ya elimu katika Uislamu.
(b) Tofautisha kati ya elimu ya mwongozo(faradh ‘Ain) na elimu ya mazingira (faradh kifaya).

6.      ‘Mgawanyo wa Elimu Dunia na Akhera (dini) haukubaliki (haupo) katika Uislamu’. Eleza ni kwa nini kwa kutoa sababu zisizopungua tano.

7.      (a)   Ni ipi elimu yenye manufaa?
(b)  Eleza kwa ufupi, kwa nini ili Uislamu usimame katika jamii, hatuna budi kutotenganisha ‘Elimu ya Mwongozo na Elimu ya Mazingira’?
BY MEEK HMK CLICKER
Share:

1 comment:

  1. This is the only page where I got the best and exactly answers to my questions. Thanks for the help. !

    ReplyDelete

KANUNI ZA KUSOMA NA KUFAULU

Kila mwanafunzi anahitaji kufaulu katika mitihani yake. Walimu nao hujisikia vizuri wakati wanafunzi wao wanapofanya vizuri katika miti...

ads

Hussein

Hussein + Hassan Mussa Kileo
Hussein Mussa. Powered by Blogger.
GOLDENTHINKERZ

Facebook

GOLDEN THINKERZ

Ask a question

Name

Email *

Message *

golden team

Powered By Blogger

Random Posts

Recent Posts

Popular Posts

AddsOn

AddsOn
AddsOn

Blog Archive

Recent Posts

Unordered List

Theme Support